Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Januari 24, 2025 Local time: 03:41

WHO yaitaka China kutoa maelezo zaidi kuhusiana milipuko ya magonjwa ya kupumua


Wasafiri wakiwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Wuhan Tianhe Aprili 10, 2020. Picha na Reuters.
Wasafiri wakiwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Wuhan Tianhe Aprili 10, 2020. Picha na Reuters.

Shirika la afya ulimwenguni limeiomba China kutoa maelezo zaidi ya ongezeko la magonjwa ya kupumua na kuripoti kuwepo homa ya mapafu kwa watoto ambayo ofisi yake ya china leo iliita ukaguzi wa kawaida.

Mamlaka za China kutoka tume ya taifa ya afya ilifanya Mkutano na waandishi wa habari Novemba 13 kutoa ripoti ya ongezeko la matukio ya ugonjwa wa kupumua.

Mamlaka zimeelezea kuongezeka huko kunaweza kuwa kumetokana na kuondolewa masharti ya COVID -19 na mzunguko wa vimelea vinavyojulikana kama vile flu , homa ya mapafu, maambukizo ya kawaida ya bakteria ambayo kwa kawaida yanaathiri watoto wadogo , virusi vinavyoshambulia mfumo wa kupumua –RSV na vile vinavyosababisha COVID.

Wote china na WHO wamekabiliwa na maswali kuhusu uwazi wa kutoa taarifa kuhusu kesi za karibuni za COVID -19 zilizotokea katika mji wa katikati wa china – Wuhan mwishoni mwa mwaka 2019.

Forum

​
XS
SM
MD
LG