Polisi wamesema kwamba karibu darzeni mbili ya watu wamefanikiwa kuogelea na kunusurika kifo baada ya meli ya mizigo MV Afsaruddin, kuigonga feri MV Ruposhi -9 kusini mashariki mwa Dhaka.
Video inayoonyesha feri hiyo ikizama ina watu wanaopiga mayowe kuomba kuokolewa.
Mkuu wa polisi Aslam Mia, amesema kwamba feri hiyo ilikuwa imebeba zaidi ya abiria 60.
Abiria 22 kati yao walifanikiwa kuogelea na kujiokoa.
Mkuu wa wilaya Monjurul Hafiz, amesema kuwa walinzi wa pwani na watu wenye ujuezi wa kuogelea wanasaidia katika kuwatafuta waathirika.
Chanzo cha habari hii ni shirika la habari la AFP