Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Machi 19, 2024 Local time: 08:02

Wanawake wanane kuhutubia Ijumaa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa


Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa
Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa

Wanawake wanane - makamu wa rais watatu na mawaziri wakuu watano - wamepangwa kuzungumza Ijumaa katika Mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, mjini New York, Marekani.

"Hatuwezi kuokoa sayari yetu ikiwa tutawaacha walio katika mazingira magumu - wanawake, na wasichana wachache," Rais wa Slovakia Zuzana Caputova aliambia mkutano mapema wiki hii.

FILE - Newly elected Slovakia's President Zuzana Caputova attends a televised debate in Bratislava, Slovakia, March 31, 2019.
FILE - Newly elected Slovakia's President Zuzana Caputova attends a televised debate in Bratislava, Slovakia, March 31, 2019.

"COVID-19 inatishia kurudisha nyuma mafanikio ambayo tumepata," Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, rais wa kwanza mwanamke wa nchi yake, aliuambia mkutano Baraza Kuu la UN Alhamisi.

Rais Samia Suluhu Hassan
Rais Samia Suluhu Hassan

Siku hiyo ya Alhamisi pia, Katibu Mkuu wa UN, António Guterres, alionya katika mkutano wa chakula ambao unataka kuboresha uzalishaji wa chakula ulimwenguni kwamba karibu nusu ya dunia haiwezi kumudu chakula bora.

Antonio Guterres
Antonio Guterres

"Chakula ni uhai. Lakini katika nchi, jamii na kaya katika kila kona ya ulimwengu, hitaji hili muhimu - haki hii ya binadamu - halijatimizwa," Guterres aliuambia Mkutano wa Mifumo ya Chakula pembeni mwa mkutano huo wa kila mwaka.

Guterres alisema kuwa watu bilioni 3 hawawezi kumudu chakula chenye lishe. "Kila siku, mamia ya mamilioni ya watu hulala na njaa. Watoto wanakufa na njaa," alisema.

Wakati mamilioni ya watu wanakufa njaa, na athari za njaa zinajidhihirisha wazi katika nchi kama Yemen na Ethiopia, karibu theluthi moja ya chakula chote kinachozalishwa hupotea au kuharibika.

XS
SM
MD
LG