Uchaguzi huu ni mmoja wa uchaguzi unaoangaliwa kwa ukaribu barani Afrika, ambapo rais aliye madarakani sasa Uhuru Kenyatta anagombania wadhifa huo akikabiliana na mpinzani wake wa siku nyingi, kiongozi wa upinzani Raila Odinga katika kiti cha urais.
Mchuano katika uchaguzi huu wa leo unaelezwa kuwa mkubwa. Rais Uhuru Kenyatta ametoa mwito kwa wapiga kura wa nchini humo kupiga kura kwa amani.
Kenyatta na Odinga waligombania urais katika uchaguzi wa mwaka 2013 na raia wengi wa Kenya wanasema kampeni za wanasiasa hao hazijawahi kumalizika.