Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Machi 28, 2023 Local time: 20:45

Taliban wamefunga kivuko kikuu kati ya Afghanistan na Pakistan - Maafisa


Maafisa wa Taliban wakiwa kwenye mpaka wa Torkham.

Kuna ripoti kuwa  Jumatatu  kumetokea ufyatuaji wa risasi, uliodumu kwa muda mfupi huko Torkham, kivuko kikuu cha mpakani kati ya Afghanistan na Pakistan. Hakuna taarifa yoyote ya vifo.

Maafisa wa Pakistani waliliambia shirika la habari la Associated Press Taliban ya Afghanistani ilifunga mpaka Jumapili kwa sababu Pakistan inadaiwa kuwazuia wagonjwa wa Afghanistan na wahudumu wao kuingia Pakistan bila hati za kusafiria.

Afisa wa mpaka wa Taliban Torkham, Mullah Mohammad Siddiq, aliwashauri raia wa Afghanistan kutosafiri kuelekea kwenye mpaka wa Torkham.

Alisema kupitia mtandao wa twitter kwamba Pakistan haikutimiza "nia yake ya dhati, lakini hakufafanua zaidi.

Taifa hilo lisilo na bahari, linashirikiana mpaka Pakistan wa takriban kilomita 2,600, wakati Torkham ni kituo kikuu cha usafiri kati ya nchi hizo mbili.

Facebook Forum

XS
SM
MD
LG