Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 25, 2024 Local time: 08:23

Shirika la Save the Children: Utapiamlo, Ukame na mizozo yaongezeka Ethiopia


FILE - Watu wakiwa karibu na mizoga ya kondoo zilizokufa kutokana na ukame katika kijiji cha Hargududo, kilomita 80 kilometers kutoka mji wa Gode, Ethiopia, April 07, 2022.
FILE - Watu wakiwa karibu na mizoga ya kondoo zilizokufa kutokana na ukame katika kijiji cha Hargududo, kilomita 80 kilometers kutoka mji wa Gode, Ethiopia, April 07, 2022.

Kiwango cha utapiamlo kote mashariki na kusini mashariki mwa Ethiopia kimeongezeka katika miezi ya hivi karibuni  wakati ukame, kukoseshwa makazi na mzozo vikiongezeka kufikia 185,000 kwa watoto ambao wanakadiriwa kutaabika na utapiamlo, shirika la save the Children limesema.

Ukame wa Muda mrefu pamoja na huduma dhaifu za afya kutokana na ukosefu wa uthabiti, janga la COVID 19, na ukosefu wa fedha vimesababisha zaidi ya watu milioni moja kuhitaji msaada wa haraka wa lishe kote somali, Oromia, SNNP na maeneo ya upande wa magharibi.

Hata hivyo hali mbaya ya utapiamlo inatarajiwa katika miezi ya hivi karibuni wakati bei ya vyakula inazidi kuongezeka kutokana na kushuka kwa thamani ya sarafu ya Ethiopia na vita vya Ukraine, huku mifugo ya familia ikiendelea kushuka thamani kutokana na ukame mkubwa katika historia kwenye pembe ya Afrika kuwahi kutokea.

Katika eneo la Somali mashariki mwa Ethiopia moja ya eneo lililoharibiwa vibaya na ukame, kiwango cha utapiamlo kwa zaidi ya miezi 12 kimeongezeka kufikia asilimia 64 ikiwa ni ongezeko la asilimia 43 kati ya mwezi januari na april pekee.

XS
SM
MD
LG