Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Mei 07, 2024 Local time: 21:06

Rwanda: Majaji wa Mahakama ya ICC waeleza utaratibu mpya wa kesi ya mshukiwa wa mauaji ya kimbari


Felicien Kabuga
Felicien Kabuga

Majaji katika Mahakama ya Uhalifu wa Kivita ya Umoja wa Mataifa wameamua mshukiwa wa mauaji ya kimbari nchini Rwanda Felicien Kabuga mwenye umri mkubwa hafai kufikishwa mahakamani.

Hata hivyo wamesema taratibu za kisheria zilizopunguzwa katika kesi ya mshukiwa huyo zinaweza kuendelea, katika uamuzi uliochapishwa leo Jumatano.

Mfanyabiashara huyo wa zamani na mmiliki wa kituo cha redio alikuwa mmoja wa washukiwa wa mwisho waliotafutwa na mahakama hiyo inayohukumu mashtaka ya uhalifu uliofanyika katika mauaji ya kimbari ya mwaka 1994, wakati Wahutu waliokuwa na msimamo mkali walipoua zaidi ya Watutsi 800,000 walio wachache na Wahutu wenye msimamo wa wastani katika siku 100.

Kabuga ni mzee mwenye umri wa zaidi ya miaka 80, ingawa tarehe yake kamili ya kuzaliwa inautata.

Alikamatwa nchini Ufaransa mwaka 2020 baada ya zaidi ya miaka 20 kukimbia.

Mahakama imetambua kuwa Bw. Kabuga hana uwezo tena wa kushiriki kikamilifu katika kesi yake, uamuzi uliochapishwa kwenye tovuti ya mahakama ya The Hague ulisema.

Uamuzi huo ulikuja baada ya madaktari kumkuta Kabuga na shida ya afya ya akili..

Chanzo cha habari hii ni shirika la habari la Reuters.

Forum

XS
SM
MD
LG