Biashara ya kusafirisha bidhaa kupitia bahari ya Black Sea imesalia imara kwa kiasi kikubwa, taarifa hiyo ilisema lakini ikaongeza kuwa hatari inayoweza kutokana na kushindwa kijeshi, na "matokeo mabaya ya kisiasa" ya Russia kushambulia meli za wafanyabiashara, zinaweza kuwa na "athari kubwa zaidi kuliko" faida yoyote kutoka kwa kizuizi cha biashara inayoenda Ukraine.
Ikulu ya Marekani iliishutumu Korea Kaskazini siku ya Ijumaa kwa kusafirisha silaha hadi Russia, karibu na mpaka wa Ukraine.
Madai yake yanatokana na picha iliyotolewa Ijumaa inayoonyesha shehena kutoka bohari ya mizigo nchini Korea Kaskazini, au DPRK, ambayo ilipakiwa kwenye meli iliyokuwa na bendera ya Russia kabla ya kuhamishwa kwa njia ya reli hadi kwenye bohari kando ya mpaka wa kusini magharibi mwa Russia.
Uwasilishaji huo ulifanyika kati ya Septemba 7 na Oktoba 1, Marekani inasema.
Forum