Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Januari 22, 2025 Local time: 14:04

Katibu mkuu wa NATO asema Ukraine inapata ushindi


Katibu mkuu wa NATO, Jens Stoltenberg, Alhamisi amesema wanajeshi wa Ukraine wanaendelea kupata ushindi katika kukabiliana na mapigano makali.

Stoltenberg, pia anatoa wito kwa washirika kutoa misaada zaidi, kuongeza utengenezaji wa silaha na kuharakisha uwasilishaji wa silaha kwa Ukraine.

Akizungumza na wanahabari mjini Kyiv, amesema kadri Ukraine, inavyozidi kuwa na nguvu, ndivyo uvamizi wa Russia unakaribia kumalizika.

Akizungumza pamoja na rais wa Ukraine, Volodymyr Zelenskyy, Stoltenberg amesema NATO imeshatoa oda ya silaha zenye thamani ya dola bilioni 2.5 kupelekwa Ukraine.

Stoltenberg amesema ni kwa maslahi ya usalama ya NATO kuipa Ukraine kile inachohitaji kushinda vita hivyo.

Na nchini Marekani, ambako serekali inatarajiwa kufungwa, msemaji wa Pentagon, Sabrina Singh, amesema juhudi za kusaidia vita vya Ukraine zinaweza kutatizwa.

Forum

XS
SM
MD
LG