Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 26, 2024 Local time: 03:32

Rufaa ya waandishi wa habari wa Mtandao wa IWACU yakataliwa


Waandishi wa mtandao wa habari huru Iwacu Burundi wanaotumikia kifungo, kutoka kushoto Christine Kamikazi, Agnes Ndirubusa, Terence Mpozenzi na Egide Harerimana leave wakiondoka mahakamani huko Bubanza, magharibi mwa Burundi, on Disemba 30, 2019. Photo by Tchandrou Nitanga / AFP)
Waandishi wa mtandao wa habari huru Iwacu Burundi wanaotumikia kifungo, kutoka kushoto Christine Kamikazi, Agnes Ndirubusa, Terence Mpozenzi na Egide Harerimana leave wakiondoka mahakamani huko Bubanza, magharibi mwa Burundi, on Disemba 30, 2019. Photo by Tchandrou Nitanga / AFP)

Mahakama ya rufaa nchini Burundi imetupilia mbali ombi la wanahabari wa nne wa gazeti la mtandaoni la Iwacu, kupinga adhabu iliotolewa na mahakama ya chini.

Katika taarifa kwa vyombo vya Habari, Iwacu imesema, “tunayo masikitiko kuwatangazia Warundi na jumuiya ya kimataifa kwamba mahakama ya rufaa imetupilia mbali rufaa yetu. Wanahabari wetu watasalia gerezani.”

Wanahabari wetu hawana hatia juu ya mashtaka yaliowakabili, tutaendelea kuomba haki itendeke na tutawasilisha kesi kwenye mahakama ya juu, limeongeza gazeti la Iwacu.

Wanahabari hao walikamatwa mwezi Oktoba mwaka 2019, wakielekzea kufanya uchunguzi kuhusu Habari ya shambulizi la kundi la waasi, katika mkoa wa magharibi mwa Burundi, Bubanza.

Baadae waendesha mashtaka waliwashutumu wanahabari hao kushirikiana na kundi la wahalifu, jambo ambalo waliendelea kukana.

Januari mwaka 2020, Mahakama ya mkoa wa Bubanza iliwahukumu kifungo cha miaka miwili na nusu na kila mmoja kulipa faini ya million 1 pesa za Burundi.

Shirika la haki za binadamu Amnesty International limeeleza masikitiko yake juu ya hatua hiyo ya mahakama ya rufaa, likisema haki haikutendeka kamwe.

Amnesty International inapendekeza wanahabari hao waachiwe huru bila masharti yoyote.

Imetayarishwa na Mwandishi wetu, Patrick Nduwimana, Washington, DC.

XS
SM
MD
LG