Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 03:41

Rais wa zamani wa Mauritania ahukumiwa kifungo cha jela


Rais wa zamani wa Mauritania Mohamed Ould Abdel Aziz
Rais wa zamani wa Mauritania Mohamed Ould Abdel Aziz

Rais wa zamani wa Mauritania, Mohamed Ould Abdel Aziz, amehukumiwa kifungo cha jela na jaji anayehusika na uchunguzi wa rushwa.

Rais huyo alikuwa chini ya kifungo cha nyumbani katika siku za nyuma.

Aziz ambaye aliongoza taifa hilo la kaskazini magharibi ya Afrika kuanzia mwaka 2008 mpaka 2019, amekuwa chini ya uchunguzi kwa mashitaka yanayo jumuisha utakatishaji fedha toka mwezi Machi mwaka 2021.

Rais wa zamani huyo amepinga shutuma hizo na kudai kwamba mashitaka hayo yamechochewa na sababu za kisiasa.

Amepinga vilevile kushiriki katika uchunguzi dhidi yake kwa kusema katiba inamlinda kutoshitakiwa akiwa yeye ni rais wa zamani.

Chanzo cha Habari : AFP

XS
SM
MD
LG