Kauli hiyo ameitoa Waziri Mkuu wa Qatar Jumanne wakati wa Mkutano wa Jukwaa la Kiuchumi la Dunia, WEF, huko Davos.
Sheikh Mohammed Bin Abdulrahman al- Thani amesema Qatar inaamini kwamba kupunguza mzozo huko Gaza kunaweza kusimamisha kuenea kwingineko.
Aliongeza kuwa hali ya sasa katika eneo ni kichocheo cha kuenea katika maeneo mengine.
Waziri mkuu wa Qatar na mambo ya nje sheikh Mohammed bin Abdulrahman alisema:
“ Sasa tunaona kuna kujibu mashambulizi kutoka Marekani na Uingereza dhidi ya Wa- Houthi, wakijaribu kuwazuiya kuvuruga biashara ya kimataifa.
lakini hili pia litasababisha hatari kubwa na kuenea zaidi. Siku zote tunajali zaidi diplomasia katika suluhu yoyote ya kijeshi na tunaamini kwamba tusizingatie sana mizozo midogo. Tulenge mzozo mkubwa. Na mara utakapoondolewa naamini kila kitu kitaondolewa."
Habari hii inatokana na vyanzo mbalimbali vya habari.
Forum