Kwa mujibu wa Haaretz, maafisa wa Israel wamemtambua mwanamme huyo aliyefyatua risasi kuwa ni Fadi Abu Shehadam, umri miaka 42, kutoka Jerusalem Mashariki “anaye julikana kuwa na mahusiano na kikundi cha Hamas.”
Tukio hilo lilitokea katika eneo maarufu ambalo ni takatifu kwa wote Wayahudi na Waislam. Linajulikana na Wayahudi kama Temple Mount na Waislam kama Noble Sanctuary.
Maafisa wa Israeli wanasema mmoja wa wale waliopigwa risasi na mshambuliaji huyo baadae alifariki kutokana na majeraha.
Shambulizi hilo la Jumapili ni la pili katika siku za karibuni. Kijana mmoja aliuawa Jumatano huko Old City baada ya kuwachoma visu maafisa wawili wa polisi wa mpakani.
Baadhi ya habari katika ripoti hii zinatokana na vyanzo vya habari vya AP na Reuters.