Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 18:07

Mwanamke Peruth Chamutai wa Uganda ashinda medali ya dhahabu katika Olympic


Courtney Frerichs wa Marekani alishinda medali ya fedha kwa kutumia saa tisa dakika nne na sekunde 79, wakati Mkenya Hyvin Kiyeng alitwaa medali ya shaba kwa kutumia saa tisa dakika tano na sekunde 39

Peruth Chamutai wa Uganda, alishinda medali ya dhahabu katika fainali za mbio za mita 800 kwa kumaliza mbio akitumia saa 9 dakika moja na sekunde 45 na kuweka rekodi mpya ya kitaifa ya Uganda katika mchakato huo.

Courtney Frerichs wa Marekani alishinda medali ya fedha kwa kutumia saa tisa dakika nne na sekunde 79, wakati Mkenya Hyvin Kiyeng alitwaa medali ya shaba kwa kutumia saa tisa dakika tano na sekunde 39. Mekides Abebe wa Ethiopia alimaliza wa nne kwa kutumia saa tisa dakika sita na sekunde 16.

Wanawake wengine wawili wa kiafrika Beatrice Chepkoech wa Kenya, ambaye ndiye anashikilia rekodi ya ulimwengu, na Zerfe Wondemagegn alimaliza wa nane.

Wakati huo huo, wanaume wa Kenya walitawala fainali za mita 800 ambapo Emmanuel Kipkurui Korir alishinda medali ya dhahabu kwa kutumia saa moja, dakika 45 na sekunde 6.

XS
SM
MD
LG