Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 08:26

Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa akamilisha ziara Sanaa


Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa akamilisha ziara Sanaa
please wait

No media source currently available

0:00 0:03:25 0:00

Mjumbe maalum wa Umoja wa mataifa kwa ajili ya Yemen, Hans Grundberg ametoa wito kwa pande zinazogombana nchini humo kuchukua hatua za dhati ili kuheshimu makubaliano ya kusitisha mapigano, ambayo yanatoa nafasi nadra ya kusitisha ghasia.

Hans Grundberg alisema hayo siku ya Jumatano akikamilisha ziara yake ya kwanza katika mji mkuu wa Yemen, Sanaa unaoshikiliwa na waasi wa kihouthi, na kukutana na viongozi wao.

Ilikuwa ziara ya kwanza ya raia huyo wa Sweden katika eneo linaloshikiliwa na Wahuthi tangu kushika wadhifa wake mwezi Septemba mwaka jana.

Akizungumza na waandishi habari mjini Sanaa Jumatano usiku, Grundberg ameonya kwamba “Ingawa tunaona makubaliano ya kusitisha mapigano yanaheshimishwa kwa jumla, lakini tunatakiwa kuzingatia changamoto zilizopo pia.

XS
SM
MD
LG