Takriban watu 7,800 wasio na makazi kwenye mji huo wenye siasa huru wamekuwa tatizo kwenye jimbo la California, wengi wao wakiishi kwenye mahema na magari.
Wamiliki wa nyumba, biashara pamoja na viongozi wanasema kwamba watu hao wanahatarisha afya pamoja na kuathiri matumizi ya maeneo ya umma kwa wakazi wengine.
Tatizo hilo pia linashuhudiwa kwenye majimbo kadhaa ya magharibi mwa Marekani wakati wanaharakati wa haki za wasio na makazi wakiwasilisha malalamiko kwenye mahakama.