Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Julai 27, 2024 Local time: 04:47

Malaysia yaendesha operesheni maalum ya kuwasaka wahamiaji


Maafisa wakagua bot iliyozama na kuua baadhi ya watu waliokuwa ndani yake, wakati baadhi ya wahamiaji hawajulikani. waliko huko Kota Tinggi, Jimbo la Johor, Malaysia Disemba15, 2021. Malaysia Maritime Enforcement Agency (MMEA)/Handout via REUTERS
Maafisa wakagua bot iliyozama na kuua baadhi ya watu waliokuwa ndani yake, wakati baadhi ya wahamiaji hawajulikani. waliko huko Kota Tinggi, Jimbo la Johor, Malaysia Disemba15, 2021. Malaysia Maritime Enforcement Agency (MMEA)/Handout via REUTERS

Malaysia imepeleka helikopta kuwasaka wahamiaji wa Indonesia ambao boti yao ilipata ajali.

Boti hiyo ilikuwa imewabeba Waindonesia 50 ili kuingia nchini Malaysia kinyume cha sheria.

Ajali hiyo ilitokea Jumatano wakati kuna hali mbaya ya hewa kusini mwa jimbo la Johor.

Idadi ya vifo ilipanda na kufikia 16 Alhamisi baada ya operesheni ya timu ya uokozi kupata miili mitano zaidi ya wahamiaji wa Indonesia kwenye ufukwe.

Wanajeshi waliokuwa wakifanya doria waligundua miili 11 kwenye ufukwe saa kadhaa baada ya ajali hiyo.

Miili ya wanaume watatu na wanawake wawili iligunduliwa Alhamisi, walinzi wa pwani wamesema.

Wahamiaji 20 bado hawajulikani walipo, na maafisa wamepeleka boti na helikopta kuwatafuta.

XS
SM
MD
LG