Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Machi 16, 2025 Local time: 19:34

Majangili wauwa vifaru 11 katika mbuga za wanyama Namibia


Serikali ya Botswana imeripoti takriban vifaru 50 wameuawa katika miezi 10 iliyopita, 04.04.2020. (Picha na AP).
Serikali ya Botswana imeripoti takriban vifaru 50 wameuawa katika miezi 10 iliyopita, 04.04.2020. (Picha na AP).

Wizara ya Mazingirira na Utalii ya Namibia  imesema imegundua mizoga ya vifaru 11 wanaotuhumiwa kuuwawa na wawindaji haramu katika hifadhi tangu mwanzoni mwa mwezi.

Imesema uchunguzi unaonyesha kwamba mizoga ya vifaru weusi kaskazini mwa hifadhi ya wanyama ya Etosha walikuwa kati ya umri wa wiki tatu na wazee.

Taarifa zinasema hii inaonyesha kuwa mapambano dhidi ya uwindaji haramu bado hayajamalizika.

Hakuna mtu yeyote aliyekamatwa kuhusiana na tukio hili, wakati ambapo uchunguzi bado unaendelea.

Wizara imeomba raia yeyote wa Namibia mwenye maelezo kutoa taarifa katika kituo cha polisi au kwenye wizara hiyo.

Jumla ya vifaru 22 wameuwawa na wawindaji haramu tangu mwanzoni mwa mwaka huu, kwa mujibu wa wizara hiyo.

XS
SM
MD
LG