Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 27, 2025 Local time: 14:04

Mahakama Kenya yaamrisha Miguna Miguna kurudishwa nchini


Miguna Miguna (kushoto) ambaye ni wakili wa mwanasiasa Raila Odinga wakati akijiapisha kwenye viwanja vya Uhuru Park mjini Nairobi Januari 30, 2018.
Miguna Miguna (kushoto) ambaye ni wakili wa mwanasiasa Raila Odinga wakati akijiapisha kwenye viwanja vya Uhuru Park mjini Nairobi Januari 30, 2018.

Mahakama Kuu nchini Kenya Jumatatu imetoa amri kwa maafisa wa Uhamiaji nchini humo kumruhusu mwanachama wa upinzani kurejea nchini baada ya kuondolewa kwa nguvu mapema mwezi Januari 2018.

Jaji wa mahakama hiyo Chacha Mwita ameiamuru idara ya Uhamiaji kumpa Miguna hati zake za kusafiria ili kumwezesha kurudi nchini Kenya mpaka hapo shauri lake litakaposikilizwa mahakamani juu ya uhalali wa uraia wake.

Miguna Miguna ambaye ni mwanachama wa Muungano wa upinzani Nasa na pia ni wakili alilazimishwa kupanda ndege na kurudishwa nchini Canada.

Kufukuzwa huko nchini kulifuatia kukamatwa kwake na kufunguliwa mashtaka ya uhaini kwa kuhusika na zoezi la kujiapisha kiongozi wa upinzani Raila Odinga.

Odinga ambaye ameendelea kusisitiza kuwa ndiye mshindi halali wa uchaguzi mkuu wa urais nchini Kenya uliofanyika mwaka 2017.

Wizara ya Mambo ya Ndani ilieleza kuwa Miguna alikana uraia wake wa Kenya baada ya kuchukua ule wa Canada miaka kadhaa iliyopita.

XS
SM
MD
LG