Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Julai 27, 2024 Local time: 04:20

Mafuriko Marekani yaua watu 10, wengine 40 hawajulikani waliko


Magari haya katika picha yamepata ajali baada ya kusombwa na maji kufuatia mvua kubwa zilizosababisha mafuriko huko Middle Tennessee, na kusababisha vifo kadhaa wakati nyumba na Barabara ziliposombwa na mafuriko.(AP Photo/Mark Humphrey).
Magari haya katika picha yamepata ajali baada ya kusombwa na maji kufuatia mvua kubwa zilizosababisha mafuriko huko Middle Tennessee, na kusababisha vifo kadhaa wakati nyumba na Barabara ziliposombwa na mafuriko.(AP Photo/Mark Humphrey).

Watu 10 wamefariki na wengine zaidi ya 40 hawajulikani walipo  tangu Jumamosi  kutokana na mafuriko makubwa yaliyotokea katika jimbo la Tennessee hapa nchini Marekani, shirika la habari la Associated Press limeripoti.

Mafuriko hayo yalitokana na mvua kubwa ambayo ilisomba nyumba na barabara za vijijini, maafisa wamesema.

Wakazi waliliambia shirika la Habari la AP kuwa ilikuwa ni tukio baya kushuhudia kutokana na wingi wa maji yaliyokuwa yanaingia ndani.

Miongoni mwa miili ya watu waliokufa iliyopatikana ni ya watoto wadogo ambao walisombwa na maji .

Gavana wa Tennessee Bill Lee aliandika katika mtandao wa Twitter jana akiwasihi wakazi kuwa waangalifu na katika hali ya tahadhari kubwa kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua nyingi.

Amesema wanafanyakazi kwa karibu sana na huduma za dharura pamoja na maafisa wa idara mbalimbali kuhakikisha usalama wa watu.

XS
SM
MD
LG