Ripoti zinasema kuwa barabara za mji mkuu wa jimbo hilo wa Zhengzhou zimesombwa maji wakati madereva wakilazimika kutembea kwa miguu huku maji yakiwafika kiunoni. Mafuriko hayo pia yanasemekana kusomba njia za reli ambazo zinategemewa kwa usafiri na watu wengi.
Watu 12 wanasemekana kufa kwenye vituo vya treni vya chini ya ardhi wakati takriban 500 waliokolewa kulingana na chombo cha habari cha serikali.
Mabwawa pamoja na hifadhi nyingine za maji zinasemekana kujaa kutokana na mafuriko hayo wakati kukiwa na wasi wasi wa kuporomoka kwa bwawa la Yihetan lililoko karibu na mji wa Louyang.
Tayari zaidi ya watu 100,000 wamepelekwa kwenye maeneo salama, wakati wanajeshi pamoja na polisi wakisaidia kupeleka misaada ya kibinadamu kwa watu walioathiriwa