Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Mei 23, 2025 Local time: 17:23

Maambukizi ya COVID-19 yafikia milioni 85.5 Duniani


Wafanyakazi katika eneo la kupima COVID-19 la Judiciary Square wakichukua maelezo ya watu wanaosubiri kupima mjini Washington, DC. Novemba 21, 2020. (Photo by MANDEL NGAN / AFP)
Wafanyakazi katika eneo la kupima COVID-19 la Judiciary Square wakichukua maelezo ya watu wanaosubiri kupima mjini Washington, DC. Novemba 21, 2020. (Photo by MANDEL NGAN / AFP)

Kituo kinacho fuatilia kesi za virusi vya Corona katika Chuo Kikuu cha John Hopkins cha Marekani, kinaripoti Ijumaa kwamba kuna kesi milioni 85.5 za COVID-19 na vifo milioni 1.8 duniani.

Marekani bado inaendelea kuwa juu kwenye orodha ya janga hili, ambapo kuna maambukizi takribani milioni 20 na vifo 345,000 vya virusi vya Corona, John Hopkins iliripoti.

India ina kesi milioni 10.2 na zaidi ya vifo 148,000, huku Brazil ikiwa na kesi milioni 7.6 na karibu vifo 195,000 kulingana na ripoti ya John Hopkins.

Watu 42 katika jimbo la West Virginia nchini Marekani walidhani wamepatiwa chanjo ya virusi vya Corona, lakini badala yake walipewa chanjo ambayo kile gazeti la The New York Times ilichofafanua kama matibabu ya majaribio ya kinga-mwili ya Monoclonal.

XS
SM
MD
LG