Ajali hiyo iliyotokea Jumapili usiku katika kitongoji cha Ondo, wakati lori hilo lilipopinduka baada ya kuserereka na kuacha barabara, polisi walisema.
"Baadhi ya watu walikwenda katika eneo la ajali na kuchota mafuta, wakati wa tukio hilo gari la mafuta lilipuka," msemaji wa polisi wa jimbo la Ondo, Fumilayo Odunlami-Omisanya alisema.
Bei ya petroli imeongezeka nchini Nigeria kwa zaidi ya mara tatu tangu kuondolewa kw a ruzuku iliyokuwepo kwa miongo kadhaa mwishoni mwezi Mei, na kuwathiri madereva na kaya pamoja na wafanyabiashara wadogo wadogo ambao wana majenereta yanayotumia petroli.
Chanzo cha habari hii ni Shirika la habari la Reuters
Forum