Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Mei 02, 2024 Local time: 04:12

Kwa Wamarekani wengi wana ndoto ya Krismas yenye mn'garo wa theluji, lakini...


Hali ya theluji inavyoweza kuwa mbaya wakati wa kipindi cha baridi nchini Marekani. Picha ya shirika la habari la Reuters.
Hali ya theluji inavyoweza kuwa mbaya wakati wa kipindi cha baridi nchini Marekani. Picha ya shirika la habari la Reuters.

Idadi kubwa ya Wamarekani walio na hamu ya kuona Krismas yenye theluji, matarajio ya hilo mwaka 2023 siyo mazuri.

Baadhi ya maeneo ya milima ya Rockies na eneo la Midwest tayari yamepata theluji au huenda yakapata theluji mpya Jumatatu, maeneo mengine ya nchi ambayo kwa kawaida yanafunikwa na theluji wakati huu wa mwaka bado yanaonekana kuwa yako nyuma kuwa na mn’garo wa theluji.

“Baadhi ya watu watapata ndoto zao, matakwa yao, na kupata Krismas yenye theluji dakika ya mwisho,” alisema Judah Cohen, mkurugenzi wa utabiri wa hali ya hewa huko katika Kituo cha Utafiti cha Verisk Atmospheric and Environmental Research. “Lakini sehemu nyingi za nchi hii zitakuwa na Krismas ya kawaida isiyokuwa na theluji.”

Kati ya maeneo ambayo yana kawaida ya kupata theluji wakati wa Desemba ni eneo la Northeast, ambako dhoruba kali ilitokea wiki hii na kuleta mvua nyingi katika eneo la michezo ya theluji, ski, ikiondoa theluji iliyokusanyika katika eneo.

Mtu akipita mbele ya bendera ya Marekani wakati theluji ikidondoka huko mji wa Manchester, New Hampshire, Feb. 5, 2016.
Mtu akipita mbele ya bendera ya Marekani wakati theluji ikidondoka huko mji wa Manchester, New Hampshire, Feb. 5, 2016.

“Haikuondoa njia zetu. Lakini ilikuwa ni mvua kubwa,” alisema Tom Day, Manager Mkuu wa Jumba la mapumziko la Gunstock Mountain Resort huko Gilford, New Hampshire.

Alikuwa akicheza katika eneo lenye theluji Jumatatu, wakati likiwa limefungwa, huku mvua yenye kijoto ya sentimeter 8.8 ikinyesha na upepo mkali ukivuma.

“Hilo ni neno lenye herufi nne, rain, katika shughuli zetu,” Day alisema.

Theluji katika maeneo mbalimbali ya Marekani iko chini sana kufuatia rikodi za kipindi hiki kwa mwaka huu, alisema Cohen, ambaye hatarajii kuwepo mabadiliko makubwa wakati wa Krismas.

Chanzo cha habari hii ni shirika la habari la AP

Forum

XS
SM
MD
LG