Jeshi la Korea Kusini limesema kaskazini ilifyatua kile kinachodhaniwa kuwa makombora mawili ya masafa mafupi kuelekea baharini upande wa mashariki.
Taarifa hiyo imeongeza kuwa makombora hayo yamefyatuliwa kutoka eneo karibu na Hamhung mji ulioko ufukweni mwa Korea Kaskazini na yalisafiri kilomita 190 kwa urefu wa kilomita 20.
Hadi sasa Korea Kaskazini imefanya mizunguuko sita ya majaribio na kufyatua takriban makombora kumi katika eneo.
Kwa mujibu wa wachambuzi haya ni makombora mengi yaliyofyatuliwa Korea Kaskazini kwa mwezi mmoja .