Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 23:41

Changamoto zinazo mkabili mtoto wa kike Kenya


Baadi ya matangazo ya kuwatahadharisha watoto wa kike vihatarishi vya maisha yao.
Baadi ya matangazo ya kuwatahadharisha watoto wa kike vihatarishi vya maisha yao.

Uwezekano wa mtoto wa kike kumaliza masomo yake nchini Kenya hukumbwa na matatizo mengi ikiwemo umaskini, ndoa za mapema na hata ukosefu wa karo.

Mashirika mengi hujitokeza kupigania haki ya mtoto wa kike kuwepo shuleni lakini vita hivyo hukumbwa na changamoto kwani wazazi wengi huonelea kuwaoza watoto wao wa kike ili kupata fedha ya kuendelea na maisha.

Baadhi ya wanafunzi walio wahi kulazimishwa kuolewa na kisha baadaye kuokolewa na shule na maafisa wa usalama wanazungumzia yale yaliyo wasibu.

Visa vya watoto wa kike kuacha masomo kwa sababu ya ndoa za mapema, ukeketaji na hata umaskini yamekuwa yakishuhudiwa sehemu za vijijini na kuwa nadra kwa visa kama hivyo kushuhudiwa mjini sehemu ambayo watu huchukulia kuwa ni kwa wasomi. Lakini sasa visa hivyo hushuhudiwa mijini.

XS
SM
MD
LG