Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Machi 23, 2025 Local time: 10:55

Ajali ya barabarani yasababisha vifo 20 Misri


Mamlaka nchini Misri zimefika katika eneo la tukio la ajali ambapo basi lilipinduka lilipokuwa linajaribu kulipita lori katika Barabara kuu iliyoko Kusini mwa Misri, Jumatano Aprili 142021, Karibu na mji wa Assiut, Misri. (Assiut Governorate media office via AP)
Mamlaka nchini Misri zimefika katika eneo la tukio la ajali ambapo basi lilipinduka lilipokuwa linajaribu kulipita lori katika Barabara kuu iliyoko Kusini mwa Misri, Jumatano Aprili 142021, Karibu na mji wa Assiut, Misri. (Assiut Governorate media office via AP)

Watu ishirini wameuawa na watatu kujeruhiwa kwenye ajali ya barabarani iliyohusisha basi na lori kwenye barabara kuu ya nyanda za juu nchini Misri, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na wizara ya afya.

Wizara hiyo imeeleza kwamba basi hilo, lililokuwa likitoka mjini Cairo, liligonga lori lililobeba saruji, ambalo lilikuwa limeegeshwa, baada ya kupata hitilafu, katika jimbo la Assiut, takriban kilomita 370 kusini mwa mji huo.

Afisi ya gavana wa jimbo hili, ilisema kuwa basi hilo lilitekekea kwa haraka, na ilikuwa ni vigumu kwa waopoaji, kuondoa miili iliyokwama mle.

Shirika la Habari la Reuters limesema kuwa ubovu wa barabara na uendeshaji holela wa magari, ni kati ya sababu kuu za ajali za mara kwa mara nchini Misri, ambazo zimesababisha vifo vya darazoni za watu katika siku za karibuni.

Mwezi jana, watu 18 walipoteza Maisha yao, baada ya basi ndogo walimokuwa, kugongana na lori, kwenye jimbo la Giza, takribana kilomita 80 kutoka mjini Cairo.

XS
SM
MD
LG