Mmoja wapo ya makampuni ya bima za Meli, Ever Given ya Uingereza UK Club, imesema mamlaka ya mfereji wa Suez ilikataa pendekezo la kumaliza madai hayo ya fidia.
Inaeleza kwamba madai hayo ambayo ni pamoja na gharama za dola milioni 300 za ziada za kuiokoa meli na milioni 300 kwa ajili ya kupoteza sifa zake ni nyingi sana na kwa sehemu kubwa hazina msingi.
Ever Given imetia nanga katika ziwa Great Biotter katikati ya njia ya mfereji huo.
Meli hiyo yenye urefu wa mita 400 iligonga mwamba na kwenda upande hapo march 23 na kuondolewa baada ya siku sitakufuatia kazi kubwa ya kuchimba na kuisukuma.
zaidi ya meli 400 zililazimika kusubiri kupita kwenye mfereji huo wenye urefu wa km 193 unaounganisha bahari za Sham na Mediterranean.