Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Machi 22, 2025 Local time: 02:17

Dhuruba ya theruji yakumba maeneo ya Kaskazini mwa China


Mitaa ya jiji la Jiuquan, ikiwa imefunikwa na theruji February 4, 2024. Picha na AFP/ China OUT.
Mitaa ya jiji la Jiuquan, ikiwa imefunikwa na theruji February 4, 2024. Picha na AFP/ China OUT.

Hali ya hewa kali iliathiri maeneo kadhaa kaskazini mwa China, kwa mujibu wa shirika la utangazaji la serikali CCTV.

Maafisa wa polisi walionekana wakiwaondoa watu kutoka kwa magari yaliyokwama huku kukiwa na dhoruba ya theluji katika jimbo la kaskazini magharibi mwa Xinjiang.

Maeneo kadhaa ya China yanakabiliana na hali ya baridi kali huku watu wakirejea kutoka kwa sherehe za wiki moja za mwaka mpya wa China, huku theluji kubwa ikinyesha katika mji wa kaskazini mashariki wa Shenyang.

Maafisa wa idara ya taifa ya hali ya hewa walitoa onyo la hali ya hewa ya baridi kali hadi kiwango chake cha pili cha juu, gazeti la Global Times lilisema, huku theluji nyingi ikitarajiwa kote nchini hadi Alhamisi (Februari 22).

Forum

XS
SM
MD
LG