Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 20:29

Museveni amteua mkuu mpya wa utawala wa jeshi la polisi


Rais wa Uganda Yoweri Museveni.
Rais wa Uganda Yoweri Museveni.

Rais wa Uganda Yoweri Museveni amemteua mkuu wa zamani wa idara ya upelelezi katika jeshi ambaye aliwekewa vikwazo na Marekani kwa madai ya uvunjanji wa haki za binadamu, kama mkuu wa utawala katika jeshi la polisi la nchi hiyo.

Meja Jenerali Abel Kandiho aitakiwa kuondoka kwenye wadhifa wake kama mjumbe wa usalama nchini Sudan Kusini, wiki mbili tu baada ya kuachishwa kazi kama mkuu wa ujasusi.

Msemaji wa jeshi la Uganda Luteni Kanali Ronald Kakurungu amesema katika taarifa “Kandiho ameteuliwa kwenye nafasi ya mkuu wa jeshi la polisi la Uganda”.

Kufikia mwezi uliopita, Kandiho alikuwa kamanda wa idara ya upelelezi katika jeshi na alikabiliwa na tuhuma kadhaa za unyanyasaji, ikiwa ni pamoja na kuwapiga watu, dhulma ya kingono na kuwapiga watu na vifaa vya umeme.

Wizara ya fedha ya Marekani ilimwekea vikwazo Kandiho mwezi Disemba mwaka jana, kwa madai ya ukiukaji wa haki za binadamu uliofanyika chini ya uongozi wake kama mkuu wa upelelezi katika jeshi la Uganda.

XS
SM
MD
LG