Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Februari 11, 2025 Local time: 04:51

Makamanda wa jeshi la Congo na Uganda watathmini zoezi la kutokomeza waasi


Jeshi la DRC (FARDC) likfanya mashambulizi dhidi ya waasi wa ADF Kivu Kaskazini, 2014.
Jeshi la DRC (FARDC) likfanya mashambulizi dhidi ya waasi wa ADF Kivu Kaskazini, 2014.

Makamanda wanao ongoza operesheni Suja huko beni Kivu Kaskazini mashariki mwa DRC ambao ni muungano wa Jeshi la Uganda UPDF na Jeshi la Congo FARDC wamekutana Mjini Beni Kivu kaskazini Jumatatu.

Makamanda hao wamekutana kufanya uchunguzi na ukaguzi wa kazi walizozifanya pamoja tangu Novemba mwaka 2021 hadi sasa huku lengo likiwa ni kuwasaka waasi wa ADF katika misitu ya Beni.

Operesheni hiyo inafanywa chini ya uongozi wa Luteni Jenarali Muhanga Kayanja kwa upande wa Jeshi la Uganda na Upande wa FARDC ukiongozwa na meja Jenerali Kamile Bombele.

Maofisa hao wamepongeza hatua na kazi ambazo zimefanyika na bado zinaendelea. Katika kikao chao wametangaza mafanikio makubwa dhidi ya waasi wa ADF .

Kuhusu mkutano huo wa kijeshi Austere Malivika alizungumuza na Mbunge wa Chama tawala, UDPS, Shabola Bintou akiwa kwenye ziara eneo la mashariki kufanya uchunguzi kuhusu kazi za usalama.

Mbunge huyo wa chama tawala cha UDPS anasema: "Makamanda hao wameamua kuendelea na operesheni za kijeshi hadi katika Mkoa jirani wa Ituri kama njia moja ya kutokomeza mauaji ya mara kwa mara yanayotekelezwa na makundi ya waasi kama Vile ya CODECO .

XS
SM
MD
LG