Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Machi 19, 2024 Local time: 09:17

Makonda : Tanzania haitambui ushoga ni haki ya binadamu


Makonda : Tanzania haitambui ushoga ni haki ya binadamu
please wait

No media source currently available

0:00 0:08:26 0:00

Tanzania imesaini Mkataba wa Kimataifa wa haki za kiraia na kisiasa, Mkataba wa Kimataifa wa haki za Kiuchumi, Kijamii na Kitamaduni, na Mkataba wa Kutokomeza Ubaguzi dhidi ya Wanawake, ambao umeweka wazi haki ya kila mtu kuwa huru bila kubaguliwa;

kuwa huru na usalama wake; kupewa haki sawa mbele ya sheria na kulindwa na sheria; kutumia faragha yake; kutoteswa wala kufanyiwa ukatili, kutofanyiwa vitendo vya kinyama au kudhalilishwa au kuadhibiwa; kuwa na haki ya huduma ya afya, na katazo la aina zote za ubaguzi dhidi ya wanawake, ikizitaka nchi zote kutokomeza unyanyapaaji na kuwahukumu kutokana na jinsia yao.

Lakini Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ameongeza kusema kuwa: “ nchi ya Tanzania haijakubali kwamba ni nchi inayokubali mashoga, na hata katika tamko la haki za binadamu, sisi hatujachukuwa ushoga ni sehemu ya haki za binadamu, vinginevyo sheria hii isingeweza kuwepo iwapo ushoga ni sehemu ya haki za binadamu.”
XS
SM
MD
LG