Wanaharakati na waandamanaji wanaopigania demokrasia Hong Kong wamepambana na polisi siku ya Ijuma Oktoba 3 na polisi walipojaribu kuchukua udhibiti wa baadhi ya majengo ya serikali.
Watetezi wa demokrasia wapambana na polisi Hong Kong

1
Waandamanaji wanaopinga kukaliwa kwa eneo la kati la Hong Kong wasimama nyuma na ukuta wa polisi kwenye barabara ya Nathan Road, mtaa wa biashara wa Mongkok, wakitaka hema zilizowekwa na watetezi wa dekomkrasia kuvunjwa. Oct. 3, 2014.

2
Mtetezi wa demokrasia aliyekati atoka damu mdomoni akishindikizwa na polisi baada ya kupigwa na wapinzani katika mtaa mkubwa wa biashawa wa Hong Kong wa Mongkok, ambako barabara kuuinadhibitiwa na watetezi wa demokrasia, Oct. 3, 2014.

3
Mtetezi wa demokrasia, kushoto, akibishana na mpinzani wa vuguvugu la Kukalia eneo la kati la Hong Kong, haonekani kwenye picha, huku akipigwa mateke na mpinzani mwengine katika mtaa wa biashara wa Hong Kong wa Mongkok, Oct. 3, 2014.

4
Mtetezi wa demokrasia akibururwa na polisi nje ya ofisi ya mtawala mkuu wa Hong Kong, Oct. 3, 2014.