Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 20, 2024 Local time: 05:25

Matukio ya 1619

Kama unapiga kura leo utampigia nani kura yako ya urais?

#voa400 : Biashara ya Utumwa yaendelea kuwa doa kwa historia ya Marekani

#voa400 : Biashara ya Utumwa yaendelea kuwa doa kwa historia ya Marekani
please wait

No media source currently available

0:00 0:03:24 0:00

Kuhusika kwa kanisa katika biashara ya utumwa jimbo la Rhode Island Marekani.

Maadhimisho ya Miaka 400 tangu watumwa wa kwanza kuwasili Marekani

Maadhimisho ya Miaka 400 tangu watumwa wa kwanza kuwasili Marekani
please wait

No media source currently available

0:00 0:02:58 0:00

Miaka 400 tangu waafrika wa kwanza waliofanywa watumwa kuwasili katika ardhi ya marekani. nchini Ghana maadhimisho haya yanaitwa “Mwaka wa Kurejea (nyumbani)” na nchi hiyo inakaribisha vizazi vya waafrika katika nchi za magharibi kwa kuwarahisishia visa na kuandaa matukio kadha kuhusu asili yao,

Mwaka huu ni 400 tangu watumwa wa kwanza kuwasili Marekani

Mwaka huu ni 400 tangu watumwa wa kwanza kuwasili Marekani
please wait

No media source currently available

0:00 0:05:18 0:00

Miaka 400 iliyopita, waafrika wa kwanza waliofanywa watumwa waliletwa marekani, wakiwasili katika koloni la kiingereza la Virginia. Kundi la kwanza lililetwa kutoka angola, baada ya kuchukuliwa na maharamia wa kiingereza kutoka meli ya kireno iliyokuwa imebeba watumwa.

#voa400 : Jinsi biashara ya utumwa ilivyoangamiza nguvu kazi Angola

Kwa karne kadhaa kuanzia mwishoni mwa miaka ya 1400, wafanyabiashara ya utumwa Wareno katika eneo ambalo ni Angola hivi leo walihusika na biashara haramu ya kusafirisha binadamu kupitia bahari ya Atlantic.

Takriban watumwa wa Kiafrika milioni 6 walitokea Angola, wengi wao walipelekwa katika makoloni ya Ureno, japokuwa baadhi yao waliishia kupelekwa Marekani Kaskazini.

Wakati baadhi ya machifu wa makabila walipata faida kwa kuuza mateka kwa wazungu waliokuwa wakifanya biashara ya utumwa, lakini wako viongozi ambao walijaribu kuwalinda watu wao.

Mayra de Lassalette na Betty Ayoub wa VOA walisafiri hadi Angola waliweza kukusanya simulizi mbalimbali juu ya mapambano makali dhidi ya biashara ya utumwa yalivyotokea. http://bit.ly/3083KTT

Wakati huohuo Ofisi ya Kumbukumbu ya Taifa Luanda, Angola inaonyesha nyaraka zilizokuwa zimehifadhiwa kwa kipindi cha miaka isiyopungua 300.

Wanahistoria wanasema kuwa Wareno waliondoka na kumbukumbu nyingi za kihistoria walipoondoka Angola baada ya nchi hiyo kupata uhuru mwaka 1975.

Pandisha zaidi

XS
SM
MD
LG