Juhudi za utawala wa Trump kuelekea kulainisha usalama wa taifa na idara za usalama Alhamisi zimepiga hatua muhimu baada ya wajumbe wa Seneti kupiga kura 51-49 za kuidhinisha Kash Patel kuwa mkuu wa Idara ya upelelezi ya Marekani, FBI.
Wahandisi wa kijeshi wa Marekani wamelenga zaidi ya miradi 600 ya nishati na miundombinu ambayo inaweza kuharakishwa chini ya mpango wa kitaifa wa Dharura ya Nishati uliotangazwa na Rias Donald Trump, kulingana na taarifa iliyochapishwa kwenye tovuti yao.
Waziri wa Ulinzi wa Marekani Pete Hegseth ameomba baadhi ya vitengo vya jeshi kupendekeza matumizi yatakayo punguzwa kama sehemu ya punguzo la asilimia 8 ndani ya kila mwaka kwa miaka 5 mitano ijayo.
Shirika la Kimataifa la Biashara, WTO Jumatano limesema kuwa mazungumzo kususu taharuki za kibiashara ni muhimu baada ya China kutuhumu Marekani kwa hatua ya kuongeza ushuru, inayoweza kuyumbisha soko la kimataifa.
UJerumani inajiandaa kwa uchaguzi mkuu Jumapili, kampeni zikiwa zimeangazia zaidi uhamiaji na gharama ya juu ya maisha.
Mwanamke wa Kiyazidi aliyenusurika ubakaji na kuzuiliwa na kundi la Islamic State huku akiokolewa kutoka Gaza Oktoba mwaka jana kupitia operesheni iliyoongozwa na Marekani, hatimaye amewasili Ujerumani.
Marekani imeongeza maradufu idadi ya wafungwa wanaodhaniwa kuwa tishio kubwa pamoja na wale wanaosubiri kurejeshwa makao kwenye kituo cha jeshi la wanamajaji la Marekani cha Guantanamo Bay nchini Cuba.
Mashambulizi kutoka kwa kundi la kijeshi la Rapid Support Forces la Sudan yameua mamia ya raia wakiwemo watoto, kwenye jimbo la White Nile, maafisa wa serikali na makundi ya haki za binadamu wamesema Jumanne.
Ghasia kati ya makundi hasimu ya magenge zimeua watu 14 mwishoni mwa wiki kwenye mji wa bandari wa Equador wa Guayaquil ambao ni kitovu cha mivutano kati ya magenge, polisi wamesema Jumatatu.
Utalawa wa Trump umeanza kufuta kazi mamia ya wafanyakazi wa idara ya safari za anga na kusababisha hali ya sintofahamu kuelekea kwa wikiendi yenye shughuli nyingi za usafiri wa anga, wiki chache baada ya ajali mbaya ya ndege mbili karibu na uwanja wa ndege wa Reagan mjini Washington DC.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio Jumatatu akiwa Saudi Arabia amefanya mazungumzo kuhusu sitisho la mapigano kati ya Israel na Hamas pamoja na hatma ya Gaza baada ya hali ya utulivu kurejea.
Nyota wa muziki, raia wa Colombia Shakira, Jumapili amelazimika kusitisha show yake huko Lima, Peru, na baadaye kupelekwa hospitalini kutokana na maumivu ya tumbo.
Mahakama ya Mauritius imemuachilia kwa dhamana Waziri Mkuu wa zamani Pravid Jugnauth, baada ya kukamatwa Jumamosi kwa tuhuma za usafirishaji haramu wa fedha, baada ya masanduku yaliojaa fedha kupatikana kwake nyumbani kufuatia msako.
Nchi nyingi washirika wa wengi wa NATO Alhamisi zimeelezea uungaji mkono wa mpango wa kuongeza matumizi ya ulinzi, huku wakisisitiza haja ya Ukraine na mataifa mengine ya Ulaya kuwa sehemu ya mazungumzo ya kumaliza vita vya Russia dhidi ya Ukraine.
Watu wenye silaha mashariki mwa Kongo waliwabaka mamia ya watoto na kuwaandikisha wapiganaji watoto katika viwango ambavyo havijawahi kushuhudiwa, shirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia watoto, UNICEF lilisema Alhamisi.
Mwandishi wa habari wa chombo cha habari dada cha VOA, Radio Free Europe/Radio Liberty, aliachiliwa kutoka Belarus Jumatano baada ya kufungwa jela kwa zaidi ya miaka mitatu. Kesi yake ilionwa na wengi kama iliyochochewa kisiasa.
Vyuo vikuu vya umma vya Malawi vimeamuru wanafunzi wote wanaofadhiliwa na USAID waondoke au watafute njia mbadala za kulipia ada iwapo wangependa kuendelea na masomo.
Rais Donald Trump Jumatano alitangaza kwamba yeye na Rais wa Russia Vladimir Putin wamekubaliana katika mazungumzo ya simu “kuanza mara moja” mazungumzo na kiongozi wa Ukraine ili kumaliza mzozo wa karibu miaka mitatu.
Rais Donald Trump amezidisha maradufu matakwa yake kwamba Mfalme Abdullah II wa Jordan aunge mkono mpango wake wa kuichukua Gaza na kuwaondoa Wapalestina kabisa.
Marc Fogel, mwalimu raia wa Marekani ambaye alikuwa anazuiliwa nchini Russia tangu Agosti 2021 kwa kuleta bangi inayoruhusiwa na madaktari nchini humo, aliachiliwa na Moscow Jumanne na alirejea nyumbani, White House ilitangaza.
Pandisha zaidi