Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 28, 2025 Local time: 15:12

Uhamiaji, gharama ya maisha ni kero kwa wapiga kura Ujerumani


Elon Musk
Elon Musk

UJerumani inajiandaa kwa uchaguzi mkuu Jumapili, kampeni zikiwa zimeangazia zaidi uhamiaji na gharama ya juu ya maisha.

Uchaguzi huo unafanyika baada ya kutokea mashambulizi, ya hivi karibuni yakiwa Munich, na mjadala mkubwa umehusu uhamiaji.

Chama cha AfD kimepata uungwaji mkono kutoka kwa bilionea Elon Musk, mshirika mkubwa wa rais wa Marekani Donald Trump.

Lakini msimamo wa chama hicho umeonekana kutowavutia wajerumani. AfD kinachunguzwa na idara ya ujasusi ya Ujerumani kwa madai ya kuwa na itikadi kali na maandamano dhidi ya wanasiasa wenye msimamo mkali yamekuwa yakiendelea Berlin na miji mingine.

Hali mbaya ya uchumi ilipelekea kuanguka kwa serikali ya muungano wa vyama vitatu, mnamo mwezi Novemba.

German Chancellor Olaf Scholz gives a speech during the 61st Munich Security Conference (MSC) in Munich, southern Germany on February 15, 2025. (Photo by THOMAS KIENZLE / AFP)
German Chancellor Olaf Scholz gives a speech during the 61st Munich Security Conference (MSC) in Munich, southern Germany on February 15, 2025. (Photo by THOMAS KIENZLE / AFP)

Kansela wa sasa Olaf Scholz, wa Social demokrats, anataka kukopa pesa zaidi ili kujaza pengo la bajeti na kuisaidia Ukraine kivita, lakini Fredrich Merz, kiongozi wa Christian Democrats, anasema Ujerumani haistahili kukopa zaidi.

Forum

XS
SM
MD
LG