Maambukizi yanaonyesha awamu mpya ya kusambaa kwa virusi hivyo, ambayo yalifikia kilele chake mwezi Februari nchini China, kabla ya kuongezeka Ulaya na Marekani.
Latin Amerika imeripoti robo tatu ya maambukizi ya watu 91,000 yaliyoripotiwa wiki iliyopita.
Ulaya na Marekani zimerekodi asilimia 20 ya maambukizi kila mmoja.
Idadi kubwa ya maambukizi imeripotiwa nchini Brazil, ambayo karibuni iliripoti maambukizi ya watu wengi kuliko Ujerumani, Ufaransa na Uingereza.
Brazil ni ya tatu duniani kuripoti idadi kubwa ya maambukizi ya virusi vya Corona baada ya Marekani na Russia.
Maambukizi yanaongezeka sana nchini Brazil kila siku na kuiweka nchi hiyo katika nafasi ya pili baada ya Marekani.
Watu 326,000 wamefariki kutokana na maambukizi ya Corona kote duniani. Zaidi ya nusu ya idadi ya vifo imeripotiwa Ulaya.
Imetayarishwa na mwandishi wetu Kennes Bwire, Washington, DC.