Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 09:23

Zaidi ya watu 330 wameuawa tangu kikundi cha IS kushambulia gereza Syria


Wapiganaji wa kikundi cha Syrian Democratic Forces (SDF) wakifanya ulinzi nje ya gereza la Ghwayran kaskazini mashariki ya prison mji wa Hasakeh, nchini Syria Januari 26, 2022, baada ya gereza hilo kuvamiwa na kikundi cha Islamic State.
Wapiganaji wa kikundi cha Syrian Democratic Forces (SDF) wakifanya ulinzi nje ya gereza la Ghwayran kaskazini mashariki ya prison mji wa Hasakeh, nchini Syria Januari 26, 2022, baada ya gereza hilo kuvamiwa na kikundi cha Islamic State.

Zaidi ya watu 300 wameuawa katika mapigano makubwa tangu kundi la wanamgambo la Islamic State walipovamia jela kaskazini mashariki mwa Syria, wafuatiliaji wa vita wamesema Jumapili.

Wapiganaji wa IS Januari walifanya shambulizi lao kubwa ambalo halijawahi kutokea kwa miaka kadhaa katika jela ya Ghwayran katika mji unaodhibitiwa na Wakurdi wa Hasakeh kwa lengo la kuwaachia huru wapiganaji wenzao na wengine kadhaa.

Idadi ya vifo katika mapigano makali tangu wakati huo imeongezeka na kufikia 332 wakati vikosi vya Syria Democratic Forces vinavyoungwa mkono na Marekani vikipata zaidi ya miili 50 usiku wa kuamkia leo katika majengo ya gereza na maeneo ya karibu, shirika linalofuatilia haki za binadamu nchini Syria limesema.

Kundi hilo lenye makao yake makuu ambalo linategemea vyanzo ndani vya Syria limesema kuwa wana jihadi 246, wapiganaji wa Kikurdi 79 na raia wengine saba wameuawa hadi sasa katika mashambulizi ya IS na mapigano mengine.

SDF ilitangaza kuwa imechukua udhibiti wa jela hiyo Jumatano lakini mapigano makali yaliendelea hadi Jumamosi kati ya wapiganaji wa kikurdi na wanajihadi karibu na gereza hilo.

Kwa mujibu wa SDF takriban wafungwa 3,500 na wapiganaji wa IS wamejisalimisha kwa vikosi vyake tangu operesheni zilipoanza tena jela.

Lakini maafisa wa Kikurdi wanakadiria kwamba kati ya wapiganaji wa IS 60 na 90 walikuwa wanashikiliwa katika jela hiyo.

XS
SM
MD
LG