Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 26, 2024 Local time: 06:13

WHO yathibitisha Beijing itapokea wachunguzi wa kimataifa wa COVID-19 Januari


Mfanyakazi akiwa katika vazi la kujilinda na COVID-19 akiwa katika soko la bidhaa za baharini lililofungwa wakati wa maambukizi ya awali ya virusi vya corona katika mji wa Wuhan, Jimbo la Hubei, China Jan. 10, 2020.
Mfanyakazi akiwa katika vazi la kujilinda na COVID-19 akiwa katika soko la bidhaa za baharini lililofungwa wakati wa maambukizi ya awali ya virusi vya corona katika mji wa Wuhan, Jimbo la Hubei, China Jan. 10, 2020.

Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema Beijing itapokea timu ya kimataifa ya wachunguzi wa COVID-19 ambao wanatarajiwa kwenda China mwezi Januari kwa ajili ya kupata taarifa kuhusu virusi vya corona, na WHO ndio itaongoza tume hiyo ya wachunguzi.

Awali, China ilipinga wito wa uchunguzi wa kimataifa kuhusu kiini cha virusi vya corona, ikisema wito huo ni dhidi ya China, lakini ilikuwa wazi kwa uchunguzi utakao ongozwa na WHO.

Lakini haijawa wazi iwapo wachunguzi hao wa WHO watasafiri kwenda mji wa Wuhan ambao ndio ulikuwa kitovu cha virusi vya corona, na mazungumzo yanaendelea kuhusu safari hiyo.

“WHO inaendelea kuwasiliana na china na kujadili juu ya timu ya kimataifa na mahali timu hiyo itatembelea”. Babatunde Olowokure, mkurungezi wa WHO anayehusika na dharura za kikanda magharibi mwa Pacific, ameuambia mkutano wa waandishi wa habari Alhamisi.

Jumatano, afisa wa WHO na wanadiplomasia waliliambia shirika la habari la Reuters kwamba tume ya WHO inatarajiwa kwenda China wiki ya kwanza ya mwezi Januari, kuchunguza kiini cha virusi vya corona.

XS
SM
MD
LG