Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 01:17

Waziri Mkuu wa Somalia atangaza hali ya dharura kutokana na ukame


FILE - Hali hii ya ukame nchini Somalia Juni 2017, yajirejea tena katika nchi hiyo. Picha hii ya zamani ilipigwa huko Wajaale, Somalia. (UNHCR/Mustafa Saeed)
FILE - Hali hii ya ukame nchini Somalia Juni 2017, yajirejea tena katika nchi hiyo. Picha hii ya zamani ilipigwa huko Wajaale, Somalia. (UNHCR/Mustafa Saeed)

Waziri Mkuu wa Somalia Mohamed Hussein Roble ametangaza hali ya dharura kutokana na nchi yake kukumbwa na ukame mkubwa.

Tangazo hilo linakuja baada ya Waziri Mkuu kuongoza kikao cha hali ya juu cha Baraza la Mawaziri Jumanne.

Ametoa wito kwa watu wa Somalia na Jumuiya ya Kimataifa kuwasaidia wale walioathiriwa na ukame.

Ukame mkubwa umepiga katika mikoa kadhaa kwenye nchi hiyo na kusababisha watu na wanyama kuwa katika hali mbaya ya kuhitaji chakula.

Katika baadhi ya maeneo, umesabisha vifo kwa watu pamoja na mifugo.

Umoja wa Mataifa unaripoti kwamba ukame umeongezeka kutokana na ukosefu wa mvua kwa mara ya tatu tangu mwaka 2020.

Takriban Wasomali milioni 3.5 tayari wanakabiliwa na ukosefu mkubwa wa usalama wa chakula, hilo ni kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa.

XS
SM
MD
LG