Katika uteuzi huo kuna jumla ya wanawake sita waliopewa nyadhifa mbali mbali katika baraza hilo.
Monica Juma ameteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Nje, Amina Mohammed ameteuliwa Waziri wa Elimu, Margaret Kobia ameteuliwa kuwa Waziri wa Vijana na Utumishi wa Umma, Racheal Omamo ameteuliwa kuwa Waziri wa Ulinzi, Sicily Kariuki ameteuliwa kuwa Waziri wa Afya na Farida Karoney ameteuliwa kuwa Waziri wa Ardhi ambaye ni mwanahabari mkongwe.
Hatua hii ni kufuatia ushindi wake Kenyatta katika uchaguzi wa urais 2017.
Mawaziri wa zamani walioteuliwa kuwa mabalozi ni Judi Wakhungu - Ufaransa, Cleopa Mailu - Umoja wa Mataifa mjini Geneva, Dan Kazungu - Tanzania, Phylis Kandie - Ubelgiji, Luxemburg na Umoja wa Ulaya na Willy Bett - India
Wengine Jacob Kaimenyi -UNESCO, Paris, na Hassan Wario - Austria.
Orodha kamili ya mawaziri :
Adan Mohammed - Viwanda
Amina Mohammed - Elimu
Charles Keter - Kawi
Eugene Wamalwa - Ugatuzi
Farida Karoney - Ardhi
Fred Matiangi - Masuala ya Ndani na Usalama
Henry Rotich - Fedha (Hazina Kuu)
James Macharia - Uchukuzi
John Munyes - Madini na Mafuta
Joseph Mucheru - Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
Keriako Tobiko - Mazingira
Margaret Kobia - Vijana na Utumishi wa Umma
Monica Juma -Mambo ya Nje
Mwangi Kiunjuri - Kilimo
Najib Balala - Utalii
Peter Munya - Jumuiya ya Afrika Mashariki
Racheal Omamo - Ulinzi
Raphel Tuju - Waziri (Bila wizara kwa sasa)
Rashid Achesa - Michezo
Sicily Kariuki - Afya
Simon Chergui - Maji
Ukur Yattany - Leba