Watu wanaotaka kujitenga katika sehemu zinazozungumza Kiingereza nchini Cameroon, wamekuwa wakipigania kuanzishwa kwa taifa huru liitwalo Ambazonia, tangu mwaka 2017.
Wamekuwa wakifanya mashambulizi, utekaji nyara na mauaji katika maeneo ya Kaskazini Magharibi na Kusini Magharibi.
Wakazi walioonekana kuwa na wasiwasi walikusanyika na kuzunguka mabaki, yaliyojaa matundu ya risasi, ya gari lililoungua katika kijiji cha Muea, eneo la Kusini Magharibi, siku ya Alhamisi, wakati wanaume wawili wakiutoa mwili uliokuwa umefungwa na blanketi.
Ndugu na jamaa waliokuwa wakilia walitambua na kuchukua miili miwili, kwa mujibu wa ripota wa Reuters katika eneo la tukio.
Wakazi walisema washambuliaji walifika mapema asubuhi, katika wiki ambayo shule zilifunguliwa baada ya mapumziko ya majira ya joto, na kwamba watu kadhaa waliuawa.
Forum