Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 23:56

Wanafunzi wakimbizi kambi ya Dadaab waonyesha maajabu


Kutoka kushoto: Abdirahman Hussein, Shaffe Abdullahi na Abdiweli Jama
Kutoka kushoto: Abdirahman Hussein, Shaffe Abdullahi na Abdiweli Jama

Vijana wawili wanaoishi katika kambi ya wakimbizi ya Dadaab nchini Kenya ni miongoni mwa wanafunzi waliopata maksi za juu katika mtihani wa kitaifa wa Sekondari (KCSE) na kujizolea alama ya B+ licha ya kukabiliwa na changamoto nyingi zilizoko kwenye kambi za wakimbizi.

Mwandishi wa idhaa ya Kiswahili VOA ameripoti kuwa vijana hao Abdiweli Jama and Abdirahman Hussein waliletwa kambini miaka 11 iliyopita baada ya kutoroka vita iliyoisambarartisha nchi ya Somalia kwa miongo kadha.

please wait

No media source currently available

0:00 0:02:38 0:00

Kwa upande wake Shaffe Abdullahi, ambaye ni mwenyekiti wa shule ya waberi, ambapo vijana hao walikuwa wanafunzi, anadai kuwa “ukosefu wa walimu , vifaa vya kusomea na hali ngumu ya maisha kambini zilikuwa ni changamoto za kutosha kwa wahitimu hao…. Hata hivyo matokeo mazuri ya vijana hao yametufurahisha.

Ameongeza kuwa: “Wanafunzi wengi hufanya vizuri katika masomo yao lakini hubakia kambini kwa kukosa msaada wa kujiunga na vyuo vikuu na hulazimika kufanya kazi ya ualimu katika shule za wakimbizi japokuwa hawajapata mafunzo yoyote ya ualimu… hivyo basi tunatoa wito kuwa tunaomba msaada ili wanafunzi hawa waliofanya vizuri watimize ndoto yao.”

Imetayarishwa na mwandishi wetu Hubbah Abdi, Kenya

XS
SM
MD
LG