Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 27, 2024 Local time: 10:02

Waislamu waanza mfungo wa Ramadhan huku wakitafakari dhiki inayo wakabili Wapalestina


Mkutano wa hadhara uliofanywa na Waislamu wa Marekani kuonyesha mshikamano na Wapalestina ukitaka kuwepo kusitishwa mapigano huko Gaza ukipita katika mitaa ya mji mkuu wa Marekani Washington, Oct. 21, 2023.
Mkutano wa hadhara uliofanywa na Waislamu wa Marekani kuonyesha mshikamano na Wapalestina ukitaka kuwepo kusitishwa mapigano huko Gaza ukipita katika mitaa ya mji mkuu wa Marekani Washington, Oct. 21, 2023.

Waislamu katika nchi nyingi ulimwenguni wameanza mwezi mtukufu  wa Ramadhani wakati nchi kadhaa za Afrika zitaanza kufunga Jumanne,  huku wakitafakari hali ngumu inayowakumba Waislamu Wapalestina huko  Gaza.

Mfalme wa Saudi Arabia Salman bin Abdulaziz ametumia kuanza kwa mwezi wa Ramadhani kutoa wito wa kukomeshwa uhalifu mbaya sana unaofanyika katika Gaza iliyokumbwa na vita.

FILE - Mfalme wa Saudi Arabia Salman bin Abdulaziz (Bandar Algaloud/Courtesy of Saudi Royal Court/Handout via Reuters)
FILE - Mfalme wa Saudi Arabia Salman bin Abdulaziz (Bandar Algaloud/Courtesy of Saudi Royal Court/Handout via Reuters)

Akizungumza kama msimamizi wa maeneo mawili matakatifu ya Kiislamu mfalme wa Saudi Arabia ametoa ujumbe wa shukrani wa ramadhani Jumapili jioni kwa Baraka ulizopewa ufalme wa Saudi arabia lakini alibainisha kuwa vita vya Gaza vitafunika mwezi wa ramadhani wa kufunga na kuomba .

Waislamu kote ulimwenguni wanasema kwamba mwaka huu utakuwa mgumu kwao kutokana na kiwango kikubwa cha mfumuko wa bei na gharama kubwa ya chakula kikuu kinacholiwa kipindi cha Ramadhan.

Wakati wa Ramadhani waislamu wanafunga kula na kunywa na kitamaduni wanakutana majira ya jioni na familia na marafiki kufungulia na wanaamini kwamba kufunga kunasafisha mwili na wakati huu inawakumbusha mateso wanayopitia masikini.

Baadhi ya taarifa za habari hii zinatokana na vyanzo mbalimbali vya habari.

Forum

XS
SM
MD
LG