Tume inayofanya uchunguzi dhidi ya tuhuma zilizoenea wakati wa utawala wa miaka nane ya Zuma huko Afrika Kusini inayojulikana kama “ state Capture”, wamesema rais huyo wa zamani aliweka maslahi ya washirika wake mafisadi mbele kabla ya nchi yake.
Zaidi ya hapo imesema, Gupta alimtambua Zuma kama mtu mwenye tabia inayoweza kutumika kinyume na Waafrika Kusini kwa ajili ya maslahi yao ya kibiashara.
Maelezo haya yalitolewa katika sehemu ya nne ya taarifa ya tume hiyo iliyotolewa Ijumaa imeonyesha jinsi Zuma alivyoajiri na kuwafuta kazi mawaziri muhimu katika uendeshaji wa uchumi wa nchi hiyo kwa amri ya familia ya Ghupta.
Zuma aliyekuwa Rais mwaka 2009 na familia ya Gupta iliyoingia kuishi Afrika Kusini mwaka 1993 wakati utawala wa wazungu wachache ulipokuwa ukiisha amekanusha kufanya makosa yoyote.