Hiyo itakuwa mara ya kwanza kwa viongozi wa Afghanistan kuhudhuria kikao cha wajumbe wa kimataifa kuhusu taifa lao, tangu katibu mkuu wa UN Antonio Guterres alipoanza mchakato huo mwaka mmoja uliopita, kwa lengo la kuimarisha namna jumuia ya kimataifa inavyotangamana na Taliban.
Zabihullah Mujahid ambaye ni msemaji mkuu wa Taliban ameambia televisheni ya kitaifa mapema Jumapili, kwamba serikali yao ilifanya mashauriano ya ndani kuhusu ajenda kwenye mkutano wa Doha ambao unafanyika kwa mwaka wa tatu, huku wakikubaliana kushiriki.
Alitetea uamuzi huo bila kutoa masharti yoyote kutoka kwa serikali yake, akisema kuwa kila mkutano unaolenga kuwezesha upelekaji wa misaada ya kibinadanu pamoja na uwekezaji ndani ya Afganistan ni muhimu.
Umoja wa Mataifa umesema kuwa kikao hicho cha 3 cha Doha kinalenga kuimarisha utangamano na Taliban na Afganistan kwa ujumla, kwa njia madhubuti na iliyoratibiwa kwa makini.
Forum