Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 21:23

Trump, Merkel wakutana kujadili masuala muhimu


Rais Donald Trump akiwa na Chansela Angela Merkel, White House, Washington, Marekani Aprili 27, 2018.
Rais Donald Trump akiwa na Chansela Angela Merkel, White House, Washington, Marekani Aprili 27, 2018.

Chansela wa Ujerumani Angela Merkel amekutana na Rais wa Marekani Donald Trump huko White House Ijumaa mjini Washington, Marekani katika mkutano wa siku moja kuboresha ushirikiano wao katika maeneo mbalimbali ya kiuchumi na kijeshi.

Ziara za viongozi zilizofululiza mjini Washington zimetafsiriwa na wengi kama ni juhudi za viongozi hao za pamoja kumshawishi Rais Trump kutotupilia mbali makubaliano ya nyuklia ya Iran na kuondoa ushuru wa kudumu kwa vyuma na aluminium kwa nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya.

Wakati mshikamano wa Trump na Macron uliojulikana kama “bromance” ukijieleza waziwazi wakati Macron alipotembelea Marekani, mahusiano ya Trump na Merkel bila ya shaka yanajulikana kuwa ya kawaida. Imeripotiwa kuwa wakati wa mkutano wao mwezi Machi 2017, Trump alionekana kujizuia kupeana mkono na Merkel, na viongozi hao hawakuzungumza kwa miezi mitano mpaka walipowasiliana Machi 1, kwa njia ya simu.

"Wakati Emmanuel Macron ni mwenye mafanikio zaidi katika kumuonyesha bashasha Rais Trump wakati wanapokutana, Angela Merkel hatumii bashasha kama ni kipaumbele chake katika mazungumzo, na badala yake husimamia misingi, maadili ya pamoja na maslahi ya pande zote," amesema Erik Jones, mkurugenzi wa Idara ya Tafiti za European na Eurasian katika chuo kikuu cha Johns Hopkins.

XS
SM
MD
LG