Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 20, 2024 Local time: 00:22

Tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 7.0 lapiga Mexico


Watu wakiwa nje ya nyumba zao baada ya tetemeko la ardhi kupiga katika mji wa Mexico City, Septemba 7, 2021. (Photo by RODRIGO ARANGUA / AFP)
Watu wakiwa nje ya nyumba zao baada ya tetemeko la ardhi kupiga katika mji wa Mexico City, Septemba 7, 2021. (Photo by RODRIGO ARANGUA / AFP)

Tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 7.0 kwa vipimo vya rikta lilipiga kusini mwa Mexico Jumanne jioni karibu na eneo la pwani la mapumziko la Acapulco, katika jimbo la Guerrero, na kusababisha kifo cha mtu mmoja.

Gavana wa jimbo la Guerrero Hector Astudillo aliiambia televisheni ya eneo hilo mtu mmoja aliangukiwa na nguzo ya umeme katika mji wa karibu wa Coyuca de Benitez.

Utafiti wa Jiolojia wa Marekani ulisema tetemeko hilo lilikuwa na ukubwa wa 7.0 na lilipiga katikati ya kilomita 17 kaskazini mashariki mwa mji wa mapumziko wa Acapulco, katika jimbo la Guerrero.

Katika ujumbe wa video, Rais wa Mexico Andres Manuel Lopez Obrador alisema hakukuwa na ripoti za uharibifu mkubwa huko Guerrero, au kwingineko katika mkoa huo, pamoja na Oaxaca, na Mexico City, ambapo watu walikuwa wakikimbia barabarani wakati majengo yalipoanza kuyumba.

XS
SM
MD
LG