Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 15:28

Polisi Tanzania yasema miili iliyookotwa bado kutambuliwa


IGP Simon Sirro
IGP Simon Sirro

Jeshi la polisi nchini Tanzania linaendelea kupeleleza tukio la kuokotwa kwa miili kadhaa katika maeneo mbalimbali, hususan katika jiji la Dar es Salaam.

“Kimsingi bado hakuna mwili hata mmoja uliotambuliwa wala ambaye amefika kutambua," alisema Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Simon Sirro.

Kamanda Sirro amesema hadi sasa hakuna watu waliojitokeza kutambua au kulalamika kwamba wamepoteza ndugu zao.

Taarifa ya jeshi hilo imesema kuwa baada ya watu kujitokeza utaratibu mwingine utaweza kufuatwa ikiwemo upelelezi wa vinasaba (DNA).

Hii inafuatia idadi kubwa ya miili inayookotwa maeneo mbalimbali.

Kwa mujibu wa jeshi la polisi miili hiyo ilikuwa iko kwenye viroba na mingine ikiwa imefungwa mawe makubwa na kamba.

Mkuu wa Jeshi hilo ameeleza changamoto ni kuwapata watu wanaothibitisha kupotelewa na ndugu zao.

Jeshi hilo tayari limetoa taarifa za kuokotwa kwa miili hiyo katika maeneo mbalimbali, hususani katika jiji la Dar es Salaam

XS
SM
MD
LG