Vyombo hivyo vinajaribu kutafuta kitu kilichopelekea mtu huyu kufanya shambulizi hili la kinyama la kigaidi katika jiji ambalo tukio kama hilo la kigaidi liliwahi kutokea wakati wa Septemba 11, 2001.
Wakati huohuo maafisa wa jiji hilo na wakazi wake wameahidi kuwa shambulizi hilo haliwezi kuwatishia wakazi wa New York.
Kitengo cha uchunguzi cha polisi walikuwa bado wako katika eneo la tukio Jumatano, wakichunguza gari iliyofanya shambulizi hilo ikiwa inatembea kwa mwendo kasi katika njia iliyotengwa kwa ajili ya wapanda baiskeli.
Tukio hilo lilitokea upande wa magharibi wa New York, na kuwagonga waliopanda baiskeli, watembea kwa miguu na hatimaye kuligonga basi la shule. Katika matukio hayo, watu wanane waliuwawa na wengine 20 kujeruhi baadhi yao vibaya sana.